Featured
Loading...

PICHA ZINATISHA SANA TAFADHALI...HUU NI UNYAMA MWANAUME AMCHOMA MKEWE SEHEMU ZA SIRI KISA....

Dada mmoja aliyejulikana kwa jina la Agness Marwa mwenye umri wa miaka 18 mkazi wa kijiji cha Mrito , wilayani Tarime.
Alifanyiwa ukatili huo na mume wake aitwae Marwa Chacha mnamo tarehe 13/7/2014, baada ya kukuta Tsh 2,000/= kwenye pochi ya mhanga.

Baada ya kumtuhumu kuwa amepewa fedha hizo na wanaume, ndipo akaamua kumpiga na kumfunga kamba na kumweka nje wakati mvua inanyeesha, kama hiyo haitoshi akaaenda jikoni na kuchukua kiginga cha moto na kuanza kumuunguza kama picha zinavyoonesha

Mtuhumiwa ametoroka, na mhanga kwa mila za kikurya alificha hilo tukio hadi tarehe 17/7/2014 ndipo akapelekwa hospitali ya Sungusungu iliyoko Nyamongo.

Kamanda wa polisi kanda maalumu anasema mtuhumiwa pamoja na mama yake wametoroka na hii ni baada ya kuchelewa kutoa taarifa.
Hata hivyo jeshi la polisi linaendelea kufanya upelelezi ili waweze kumkamata mthumiwa na kumpeleka kwenye vyombo vyenye Mamlaka. 

Shirika la sheria na haki za binadamu Tarime(SHEHABITA) linaendelea kufuatilia tukio hili kwa karibu na kutoa rai kwa wananchi kuacha kufanya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright entertainment | Designed By Code Nirvana
Back To Top